Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Usiku kucha uamukeamuke na kulia. Umufungulie Yawe yanayokuwa ndani ya moyo wako. Umwinulie mikono yako kwa kuwaombea watoto wako, watoto wanazimia na njaa popote katika barabara.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:19
31 Referans Kwoze  

Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Moyo wangu unakutamani usiku kucha, nafsi yangu inakutafuta kwa moyo. Utakapohukumu dunia, watu wote katika ulimwengu watajifunza haki.


Ninamulilia Yawe kwa sauti kubwa, ninamusihi Yawe kwa sauti kubwa.


Kesho yake asubui kulipokuwa kungali giza, Yesu akaamuka, akatoka katika muji na kwenda pahali penye ukiwa, kule akaanza kuomba.


Lakini Hana akamujibu: “Sivyo bwana wangu. Mimi ni mwanamuke mwenye taabu sana; mimi sijakunywa divai wala kinywaji kikali, lakini nimekuwa nikimutolea Yawe yanayokuwa ndani ya roho yangu.


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Ilipokaribia saa sita za usiku, Gideoni na kundi lake la watu mia moja wakafika kwa mwisho wa kambi, kwa mwanzo wa zamu ya kati. Wakati walipokuwa wamebadilisha wenye zamu, wakakaribia kambi ya waadui. Wakapiga baragumu na kuvunja mitungi waliyokuwa nayo.


Mafuriko juu ya mafuriko yananguruma, mawimbi na zoruba yako vinanifunika.


Katika siku zile, Yesu akapanda juu ya kilima kwenda kuomba na kukesha usiku wote akiomba Mungu.


Basi muangalie sababu hamujui wakati bwana wa nyumba atakaporudi: labda magaribi, au katikati ya usiku, au wakati jogoo anapowika, au asubui.


Ilipokuwa karibu na mapambazuko, Yesu akawafikia wanafunzi wake, akitembea juu ya maji.


Usiku ninakukumbuka, ee Yawe, na kushika sheria yako.


Sikiliza sauti ya ombi langu, ninapokulilia unisaidie, ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.


Wakati huo nitaiachilia mishale yangu mikali ya njaa iwachome na kuangamiza wakaaji wako. Nitawafanya wakufe na njaa kwa kuiharibu akiba yao ya chakula.


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


Muinue mikono kuelekea pahali patakatifu, na kumutukuza Yawe!


Wema wako ni bora kuliko maisha. Nitakusifu kwa midomo yangu.


Kuugua ndicho chakula changu. Malalamiko yangu yanatiririka kama maji.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika kule Misipa. Walichota maji na kuyamimina mbele ya Yawe, wakafunga kula chakula siku ile yote na kusema: “Tumetenda zambi mbele ya Yawe.” Samweli akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kule Misipa.


Hata hivyo, ulikamatwa mateka, watu wake wakapelekwa katika uhamisho. Hata watoto wake walipondwapondwa katika maingilio ya kila barabara; watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura, wakubwa wake wote walifungwa minyororo.


Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?


Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”


Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu.


Kifo kimetuingilia katika madirisha yetu, kimetupangia katika nyumba zetu nzuri; kimewaangukia watoto wetu katika barabara, nao vijana wetu katika viwanja vya makutano.


Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.


Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite