Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Ee Sayuni, umulilie Yawe! Machozi yatiririke kama muto muchana na usiku! Lia na kuomboleza bila kupumzika!

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:18
14 Referans Kwoze  

Ninakulilia kwa moyo wangu wote; unijibu, ee Yawe, nifuate masharti yako.


Yawe alikusudia kuubomoa ukuta wa Sayuni; aliupima na kuhakikisha kila kitu kwamba kimeharibika; minara na kuta za inje ya muji akazifanya ukiwa, zote kwa pamoja zikaangamia.


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


Heri ningepata kibanda cha wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kujiendea. Wote ni wazinzi, ni kundi la watu waasi.


Macho yangu yanatiririka machozi kama muto, kwa sababu watu hawaishiki sheria yako.


Ndiyo maana hata mawe yatalalamika juu ya ukuta, na miti ya nyumba itayaunga mukono.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Unalia usiku kucha; machozi yanatiririka juu ya mashavu yake. Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji. Rafiki zake wote wameudanganya; wamekuwa waadui zake.


Hivi ndivyo utakavyowaambia: Heri macho yangetoa machozi usiku na muchana, wala yasikome kutiririka, maana, watu wangu wamepata hasara kubwa, wameumizwa kidonda kikubwa sana.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite