Maombolezo 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Waadui zako wote wanakuzomea, wanakupigia muunzi na kukusagia meno, nao wanasema: Tumemwangamiza! Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu sasa imefika na tumeiona!
Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.
Kwa hiyo, wewe Ezekieli, toa unabii useme kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Watu wamewafanya ninyi milima ya Waisraeli kuwa tupu na kuwashambulia kutoka kila upande hata mumekuwa mali ya mataifa mengine, mukakuwa kitu cha kusimangwa na kuchekelewa kati ya watu!
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu Wafilistini walifanya kisasi, wakawalipiza kisasi waadui zao kwa ubaya sana na kuendelea kuwa waadui zao siku zote,
Uwaambie Waamoni hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe: Ninyi mulifurahia kuona hekalu langu likichafuliwa, inchi ya Waisraeli ikiangamizwa na watu wa Yuda wakipelekwa katika uhamisho.
Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.
Watu wote waliowakuta waliwaua, na waadui zao wamesema: Sisi hatuna kosa, maana hao wamemukosea Yawe anayekuwa makao yao ya kweli; Yawe ambaye ni tegemeo la babu zao!
Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.
basi, nitaiharibu nyumba hii kama nilivyoharibu ile ya Shilo, na nitaufanya muji huu kuwa mufano kwa mataifa yote ya dunia yatakaoutumia kwa kutoa laana.
Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.
Utakuwa kitu cha kuzarauliwa na cha haya, mufano wa kitu cha kuchukiza kwa makabila yanayokuzunguka, wakati nitakapotimiza hukumu zangu juu yako kwa hasira na kasirani yangu kali. Ni mimi Yawe ninayasema hivyo.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Utakunywa toka kikombe cha dada yako; kikombe kikubwa na kirefu. Watu watakuchekelea na kukuzarau; na kikombe chenyewe kimejaa.