Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wanawalilia wamama zao: Chakula kiko wapi, kinywaji kiko wapi? Wanazimia kama wale walioumizwa katika barabara za muji, na kukata roho katika mikono ya wamama zao.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:12
9 Referans Kwoze  

Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.


Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.


Sasa sina nguvu yoyote ndani ya nafsi yangu; siku za mateso zimenipata.


Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Watakula mazao yenu na chakula chenu; watawaua wana na wabinti zenu. Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe; wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini. Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea, wataiharibu kwa silaha zao.


Midomo ya watoto wachanga imekauka kwa kiu, watoto wanaomba chakula, lakini hakuna anayewapa.


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula; wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula, kusudi wajirudishie nguvu zao. Nao muji unalia, Ee Yawe, uniangalie, ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite