Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:11
26 Referans Kwoze  

Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani. Roho yangu imechafuka, moyo wangu unaugua maana nimekuasi vibaya. Kule inje kumejaa mauaji, ndani nako ni kama kifo tu.


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


akanipiga mishale kutoka kila upande. Amenipasua figo bila huruma, na nyongo yangu akaimwanga chini.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Ndiyo maana ninawaambia ninyi: musijali chochote juu yangu, muniache nilie machozi ya uchungu. Musijisumbue kunifariji kwa ajili ya kuangamizwa kwa watu wangu.


Wanafungua vinywa vyao kama simba, tayari kushambulia na kurarua.


Ninatabanika kwa kulia kwa uchungu; usiku ninalowanisha kitanda changu kwa machozi; kwa kulia kwangu ninalowanisha matandiko yangu.


Kwa maana siku zitakuja wakati watu watakaposema: ‘Heri wanawake wanaokuwa tasa, wale waliokosa kuzaa na kunyonyesha!’


Sasa, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Mbona munajiletea maovu makubwa namna hii, na kujiangamiza ninyi wenyewe, wanaume kama vile wanawake, watoto wadogo na wachanga, hata kusibaki mutu katika inchi ya Yuda?


Hivi ndivyo utakavyowaambia: Heri macho yangetoa machozi usiku na muchana, wala yasikome kutiririka, maana, watu wangu wamepata hasara kubwa, wameumizwa kidonda kikubwa sana.


Sikiliza kilio cha watu wangu, kutoka kila upande katika inchi. Yawe hayuko tena katika Sayuni? Mufalme wa Sayuni hayuko tena? Lakini Yawe anasema: Mbona wamenikasirikisha na sanamu zao za kuchongwa, nayo miungu yao ya kigeni?


Ninazama ndani ya matope mengi, hakuna pahali pa kuweka miguu. Nimetumbukia kwenye shimo refu la maji, ninachukuliwa na maji mengi.


Wewe haukunitoa katika mikono ya waadui zangu; lakini umenisimamisha kwenye pahali pa usalama.


Halafu Daudi na watu wake wakaanza kulalamika, wakalia mpaka walipoishiwa nguvu.


Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!


Moyo wangu unahangaika wala hautulii hata kidogo. Siku za mateso zimenipata.


Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa; hakuna uzima katika mwili wangu.


Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Ninauliza: “Utakuja wakati gani kunifariji?”


Kwa ajili ya hiyo tumeugua ndani ya moyo, kwa ajili ya hiyo macho yetu yamefifia.


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula; wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula, kusudi wajirudishie nguvu zao. Nao muji unalia, Ee Yawe, uniangalie, ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite