Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Malaki 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Munaponitolea sadaka ya nyama anayekuwa kipofu, au kilema, au mugonjwa, huo si uovu? Mutawala atapendezwa au kukutendea mema ukimupa zawadi ya nyama kama yule? –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.

Gade chapit la Kopi




Malaki 1:8
10 Referans Kwoze  

Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Akupelekee musaada kutoka katika hekalu lake; akukinge tokea kwenye mulima Sayuni.


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Munalizarau kwa kunitolea kwenye mazabahu yangu sadaka ya chakula kichafu. Lakini ninyi munauliza: Tumekichafua namna gani? Munakichafua kwa kuizarau mazabahu yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite