Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Malaki 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?

Gade chapit la Kopi




Malaki 1:6
52 Referans Kwoze  

“Sababu gani munaniita ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamufanyi yale ninayowaamuru?


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Na ikiwa katika maombi yenu munamwita “Baba” yule anayehukumu kila mutu pasipo upendeleo kufuatana na matendo yake, basi muishi katika heshima mbele yake kwa muda unaowabakilia kwa kuishi hapa katika dunia.


Efuraimu ni sawa na muchuuzi anayetumia vipimo vya udanganyifu, anayependa kudanganya watu.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


“Heshimu baba yako na mama yako.” Hii ni amri ya kwanza ambayo waliongeza ahadi hii juu yake:


Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Basi muangalie namna munavyopaswa kusema munapoomba: ‘Baba yetu unayekuwa mbinguni, Jina lako litukuzwe;


Kuna watu ambao wanalaani baba zao, wala hawana shukrani kwa mama zao.


“Uheshimu baba yako na mama yako, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru, kusudi uishi maisha marefu na kufanikiwa katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Unajua jinsi amri zinavyosema kwamba: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, uwaheshimu baba yako na mama yako.’ ”


uwaheshimu baba yako na mama yako na kumupenda mwenzako sawa wewe mwenyewe.”


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Makuhani wao wanavunja sheria zangu, na kukufuru vyombo vyangu vitakatifu. Hawapambanui kati ya vitu vitakatifu na vitu visivyokuwa vitakatifu, wala hawafundishi watu tofauti kati ya mambo yanayokuwa machafu na yanayokuwa safi. Wameacha kuzishika Sabato zangu, na kunizaraulisha kati yao.


Manabii na makuhani, wote hawamwogopi Mungu, uovu wao nimeuona hata ndani ya nyumba yangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


basi, hapaswi tena kumusaidia baba yake. Hivi munazarau Neno la Mungu kwa kufuata desturi zenu.


Lakini ninyi makuhani mumegeuka na kuacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mumelivunja agano nililofanya nanyi.


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


Mukuwe wenye huruma, kama vile Baba yenu anavyokuwa mwenye huruma.


Maana Musa alisema: ‘Uwaheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Anayemutukana baba yake au mama yake, anapaswa kuuawa.’


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Unajua jinsi amri zinavyosema kwamba: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, uwaheshimu baba yako na mama yako.’ ”


Kwa maana Mungu alisema: ‘Uwaheshimu baba yako na mama yako.’ Naye alisema vilevile: ‘Anayelaani baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


kule katika jangwa ambako muliona jinsi alivyowabeba safari hiyo yote kama vile baba anavyobeba mwana wake, mpaka mukafika hapa.


Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.


Taji la sifa la wazee ni wajukuu wao. Heshima ya wana ni baba yao.


Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.


Na sasa hivi tu unanililia, ukisema: Wewe ni baba yangu, ulinipenda tangu utoto wangu?


Wana wa Yonadabu mwana wa Rekabu wameshika amri waliyopewa na babu yao; lakini ninyi hamukunitii.


Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu. Makuhani wake wamevichafua vitu vitakatifu na kuivunja sheria kwa nguvu.


Yawe wa majeshi anawaambia makuhani: Sasa enyi makuhani, ninawaamuru hivi:


Sisi wote si watoto wa baba mumoja? Sisi wote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalizarau agano Yawe alilofanya na babu zetu?


Munaweza namna gani kumulipa hivyo Yawe, enyi watu wapumbafu na wasiokuwa na akili? Yeye siye baba yenu aliyewaumba, aliyewafanya na kuwaimarisha?


Ole kwake mutu anayemwambia baba: Umezaa nini? au anayemwambia mama: Umeleta nini katika dunia?


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite