Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Malaki 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa neno la Yawe lililowafikia Waisraeli kwa njia ya Malaki.

Gade chapit la Kopi




Malaki 1:1
9 Referans Kwoze  

Haya ni maono ambayo nabii Habakuki aliyofunuliwa na Mungu.


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,


Katika siku makumi mbili na moja, mwezi wa saba mwaka uleule, neno la Yawe lilifika kwa njia ya nabii Hagai na kusema hivi:


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Ujumbe wa Mungu juu ya Ninawe. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkosi.


Yawe akaniambia: Mutu yeyote, akuwe nabii au kuhani akikuuliza “Uko wapi muzigo Yawe anaotubebesha?”, wewe utawaambia: Ninyi ndio muzigo kwa Yawe, naye atawatupa mbali. –Ni ujumbe wa Yawe!–


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite