Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 9:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 “Munitegee sikio vizuri: Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu.”

Gade chapit la Kopi




Luka 9:44
26 Referans Kwoze  

Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Naye akaongeza kuwaambia: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


Lakini Maria akachunga mambo hayo yote ndani ya moyo na kuyafikiri sana.


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Lakini ninawaambia maneno haya kusudi wakati ule utakapotimia mupate kukumbuka kwamba nimekwisha kuwaambia. “Sikuwaambia ninyi maneno hayo mbele kwa sababu nilikuwa ningali pamoja nanyi.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Halafu Yesu akawatwaa wanafunzi wake kumi na wawili pembeni, akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema, na maneno yote yaliyoandikwa na manabii juu ya Mwana wa Mutu yatatimizwa.


Basi Yesu akarudia Nazareti pamoja nao, akaendelea kuwatii. Na mama yake alichunga maneno haya yote katika moyo wake.


Na wote waliosikia habari ile wakafikiri juu yake na kujiuliza: “Mutoto huyu atakuwa mutu gani?” Maana hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.


kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akiwaambia: “Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu, nao watamwua, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Kisha Yesu akaanza kuwafundisha wanafunzi wake, akisema: “Sherti Mwana wa Mutu ateswe na kukataliwa na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani pamoja na walimu wa Sheria. Atauawa na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka.”


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.


Daudi akamujibu Gadi: “Nina mashaka makubwa! Lakini afazali kuazibiwa na Yawe, kuliko kutiwa katika mikono ya watu, maana yeye ana rehema sana.”


Yesu akawauliza: “Munaamini sasa?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite