Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 9:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Nao wakajibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji, wengine wanasema kwamba wewe ni Elia, na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”

Gade chapit la Kopi




Luka 9:19
12 Referans Kwoze  

Halafu wakamwuliza: “Basi wewe ni nani? Wewe ni Elia?” Yoane akajibu: “Mimi si yeye.” Wakamwuliza tena: “Wewe ni yule nabii?” Naye akawajibu: “Hapana.”


Lakini wengine walisema: “Huyu ni nabii Elia.” Wengine walisema: “Yeye ni nabii sawa na mumoja wa wale manabii wa zamani.”


Halafu akawaambia wasimamizi waliokuwa chini yake: “Mutu huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”


Wafarisayo wakamwuliza tena yule aliyekuwa kipofu: “Na wewe unasema nini juu ya yule aliyekuponyesha macho?” Akajibu: “Yeye ni nabii.”


Watu wamoja katika kundi lile waliposikia maneno hayo, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye Nabii aliyepaswa kuja!”


Wakamwuliza Yoane: “Ikiwa wewe si Kristo, wala Elia, wala yule nabii, basi sababu gani unabatiza?”


Katika siku zile Yoane Mubatizaji alitokea akihubiri katika jangwa la Yudea


Mufalme Herode alisikia habari za Yesu, kwa maana jina lake lilikuwa limevuma fasi zote. Watu wamoja walisema: “Huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”


Siku moja Yesu alipokuwa akiomba kwenye nafasi ya upekee, nao wanafunzi wake wakiwa pale karibu naye, akawauliza: “Watu wanasema kwamba mimi ni nani?”


Na halafu Yesu akawauliza: “Na ninyi munasema kwamba mimi ni nani?” Petro akamujibu: “Wewe ni Masiya wa Mungu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite