53 Nao wakamuchekelea kwa sababu walijua kwamba amekwisha kufa.
Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.
Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.
Yesu akasema: “Muondoshe jiwe hili!” Marta, dada wa yule marehemu, akamujibu: “Bwana, anaanza sasa kunuka, kwa maana ni siku ine sasa tangu alipozikwa!”
Lakini mimi ni mududu tu, wala si mutu; nimetukaniwa na kuzarauliwa na watu.
Kweli wanaonichekelea wamenizunguka, matusi yao yananizuiza kulala.
Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake. Sasa, watu wananichekelea. Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.
Halafu akasema: “Mutoke hapa. Binti huyu mudogo hakukufa, lakini analala tu.” Nao wakaanza kumuchekelea.
Watu wote walikuwa wakilia na kusikitika sana kwa ajili ya kifo cha mutoto. Lakini Yesu akasema: “Musilie, kwa maana hakufi, lakini analala tu!”
Lakini Yesu akamushika mukono na kumwambia kwa sauti kubwa: “Mutoto, simama!”