Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 8:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Watu wote walikuwa wakilia na kusikitika sana kwa ajili ya kifo cha mutoto. Lakini Yesu akasema: “Musilie, kwa maana hakufi, lakini analala tu!”

Gade chapit la Kopi




Luka 8:52
14 Referans Kwoze  

Wakati Yesu aliposikia habari hii, akasema: “Tukio la ugonjwa huu si la kumwua, lakini shabaha yake ni kuonyesha utukufu wa Mungu na kusudi Mwana wa Mungu atukuzwe.”


Kundi kubwa la watu walimufuata. Kati yao kulikuwa wanawake waliokuwa wakijipigapiga kwenye kifua kwa huzuni na kumulilia.


‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Utukufu wa Yawe ukaonekana mbele ya macho ya watu wa Israeli kama moto unaowaka juu ya mulima.


Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.


Yesu alipofika ndani ya nyumba ya Yairo, hakuruhusu mutu kuingia pamoja naye isipokuwa Petro, Yoane, Yakobo, baba na mama wa mutoto.


Nao wakamuchekelea kwa sababu walijua kwamba amekwisha kufa.


Nalo kundi la watu waliofika kuangalia mambo yale, wakaona yote yaliyotokea. Kwa hiyo, wakarudia wakijipigapiga kwenye kifua kwa huzuni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite