Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 8:47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

47 Yule mwanamuke alipoona kwamba ametambulikana, akakuja akitetemeka kwa woga na kujitupa mbele ya Yesu. Na pale mbele ya watu wote, akaeleza sababu gani alimugusa na namna alivyoponyeshwa mara moja.

Gade chapit la Kopi




Luka 8:47
18 Referans Kwoze  

Yule mwanamuke akaogopa na kuanza kutetemeka, kwa sababu alitambua yote yaliyomutukia. Halafu akakuja kujitupa kwa miguu yake na kumwambia ukweli wote.


Mapendo yake kwa ajili yenu yanazidi kuongezeka anapokumbuka vile mulivyokuwa tayari kumutii na vile mulivyomupokea kwa woga na kutetemeka.


Basi kwa kuwa tunakubaliwa kuwa washiriki wa ufalme usioweza kutikiswa, tukuwe watu wenye shukrani. Tuonyeshe shukrani ile kwa kumwabudu Mungu kwa njia inayomupendeza kwa heshima na woga,


Sababu ya hii nilikuwa kwenu katika hali ya uzaifu na woga, mwenye kutetemeka sana.


Mumutumikie Yawe kwa woga; muiname mbele ya mwana wake na kutetemeka, kusudi asikasirike, nanyi musiangamie kwa rafla; kwa maana hasira yake inawaka haraka. Heri wote wanaokimbilia kwake!


Basi yule mulinzi akaomba wamuletee taa, akarukia mbio ndani, akajitupa mbele ya Paulo na Sila, akitetemeka kwa hofu.


Samweli akafanya sawa alivyoambiwa na Yawe, akaenda Betelehemu. Wazee wa muji wakatoka kwenda kumupokea wakiwa wanatetemeka, wakamwuliza: “Umekuja kwa amani?”


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nimeregea na kupondekanapondekana; ninaugua kwa kusongwa katika moyo.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Basi wale wanawake wakaondoka upesi kutoka kwenye kaburi, wakijazwa na woga na furaha kubwa vilevile. Wakakimbia kwenda kuwapasha wanafunzi wake habari ile.


Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka; Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli, lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.


Ninawajua watu wa Efuraimu, Waisraeli hawakufichwa kwangu. Ninyi watu wa Efuraimu mumefanya uzinzi, watu wote wa Israeli wamejichafua.


Enyi munaomwabudu Mungu, mukuje wote musikilize, nami nitawaelezea mambo aliyonitendea.


Lakini Yesu akasema: “Kuna mutu aliyenigusa kwa maana nimejisikia kwamba nguvu zimenitoka.”


Na Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite