Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 8:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Basi pepo wakamutoka mutu yule na kuingia ndani ya wale nguruwe. Kundi zima la nguruwe wakatelemuka mbio kwenye mulima na kutumbukia ndani ya maji, nao wakazama.

Gade chapit la Kopi




Luka 8:33
8 Referans Kwoze  

Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Na Yesu akawaambia: “Mwende!” Basi wakatoka ndani ya wale watu na kuingia ndani ya nguruwe. Mara moja kundi zima likatelemuka mbio toka kwenye maporomoko ya mulima na kujitupa ndani ya ziwa nao wakazama ndani ya maji.


Siku moja, Yesu alisimama pembeni ya ziwa la Genezareti na watu wengi walimusongasonga kusudi wasikie neno la Mungu.


Na karibu na pale kulikuwa kundi la nguruwe wengi waliokuwa wakijitafutia chakula kwenye mulima. Wale pepo wakamusihi Yesu awaruhusu kuingia ndani ya wale nguruwe. Naye akawaruhusu.


Wachungaji wa nguruwe walipoona jambo lililotokea, wakaenda mbio kupasha habari katika muji na katika vijiji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite