Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 8:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Nao wale pepo walimusihi Yesu kwamba atakapowafukuza asiwaamuru kutumbukia ndani ya shimo lisilokuwa na mwisho.

Gade chapit la Kopi




Luka 8:31
14 Referans Kwoze  

“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Yule nyama uliyemwona alikuwa yuko zamani, lakini sasa hayuko tena. Naye ni tayari kupanda toka katika shimo la kuzimu na kwenda kuangamizwa kabisa. Nao wakaaji wa dunia ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangia kuumbwa kwa dunia, watashangaa wakati watakapomwona yule nyama, kwa sababu alikuwa yuko zamani lakini hayuko sasa, naye atatokea tena!


Wakati watakapomaliza kutoa huo ushuhuda wa Mungu, yule nyama wa ajabu anayetoka katika kuzimu atapigana vita nao, naye atawashinda na kuwaua.


Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).


Wakati alipomwona Yesu, akalalamika na kuanguka mbele yake, na kusema kwa nguvu: “Yesu, Mwana wa Mungu Mukubwa, kuna neno kati yako na mimi? Ninakusihi, usinitese!”


Lakini sasa, unyooshe mukono wako umuguse mwili wake. Utaona namna atakutukana waziwazi.”


Lakini sasa, unyooshe mukono wako uguse mali yake. Utaona namna atakutukana waziwazi!”


Na karibu na pale kulikuwa kundi la nguruwe wengi waliokuwa wakijitafutia chakula kwenye mulima. Wale pepo wakamusihi Yesu awaruhusu kuingia ndani ya wale nguruwe. Naye akawaruhusu.


Wala usijiulize: “Ni nani atakayeshuka katika kuzimu?” (maana yake kumupandisha Kristo toka kule kwenye wafu).


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite