Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 8:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Yesu akamwuliza: “Jina lako nani?” Naye akamujibu: “Jina langu ni ‘Jeshi.’ ” Alisema vile kwa sababu ndani ya mutu yule mulikuwa pepo wengi.

Gade chapit la Kopi




Luka 8:30
7 Referans Kwoze  

Haujui kwamba ninaweza kumwomba Baba yangu musaada na mara moja angenitumia zaidi ya makundi kumi na mawili ya wamalaika?


pamoja na wanawake wamoja ambao alikuwa ameondosha pepo ndani yao na magonjwa mengine. Kati ya wale wanawake kulikuwa Maria (aliyeitwa wa Magdala), aliyekuwa ameponyeshwa pepo saba;


Yesu alipokwisha kufufuka asubui mapema, siku ya kwanza ya juma, alimutokea kwanza Maria wa Magdala, yule aliyefukuza pepo saba toka ndani yake.


Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”


Basi Yesu akamwuliza: “Jina lako nani?” Naye akamujibu: “Jina langu ni ‘Jeshi’, maana sisi ni wengi.”


Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.


Alisema vile kwa sababu Yesu alikuwa amemwamuru huyo pepo, atoke ndani ya yule mutu. Huyo pepo alimukamata mutu yule mara nyingi, na ijapokuwa watu walimufunga na minyororo na vifungo vya chuma kusudi asitoroke, yeye alivikata. Na yule pepo alimusukuma kwenda katika jangwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite