20 Halafu watu wakamwambia Yesu: “Mama yako na wandugu zako wanasimama inje, wanataka kukuona.”
Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.
Au sina haki ya kusafiri pamoja na mwanamuke mukristo kama vile mitume wengine wanavyofanya, nao wandugu za Bwana na hata Petro?
Hawa wote walikuwa wakikusanyika kwa nia moja kwa kuomba, pamoja na wanawake wamoja, Maria mama wa Yesu, na wandugu za Yesu.
Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.
Mama na wandugu za Yesu wakakuja kumwona, lakini hawakuweza kufika karibu naye kwa ajili ya kundi kubwa la watu.
Lakini Yesu akawajibu: “Mama yangu na wandugu zangu ni wale wanaosikia neno la Mungu na kulishika.”