Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Ndiyo sababu nilijiona kwamba sistahili kuja kwako. Lakini sema neno tu, na mutumishi wangu atapona.

Gade chapit la Kopi




Luka 7:7
10 Referans Kwoze  

Kwa neno lake aliwaponyesha, akawaokoa wasiangamie.


Watu wote wakashangaa sana na kusemezana: “Hatujaona mambo kama haya! Mutu huyu anawaamuru pepo kwa mamlaka na uwezo wake, nao wanatoka!”


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akapona ukoma.


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Halafu Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu na kwa yule mukubwa wa waaskari, yule mukubwa akawatuma warafiki zake kumwambia Yesu: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu.


Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena niko na waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’ naye anakwenda! Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’ naye anakuja! Nami nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’ naye anafanya vile!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite