45 Wewe haukunibusu kwa kunisalimia, lakini mwanamuke huyu hakuacha kubusu miguu yangu tangu nilipoingia humu.
Zaidi ya hayo, Abusaloma alinyoosha mukono wake akamukumbatia na kumubusu mutu yeyote aliyekuja kuinama mbele yake.
Musalimiane kwa upendo wa kikristo. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimia.
Mufalme akamwambia: “Kimuhamu atakwenda nami, na nitamutendea lolote unaloona ni zuri. Na lolote utakalotaka nikutendee, nitakutendea.”
Musalimiane kwa upendo wa kikristo.
Wandugu wote wanaokuwa hapa wanawasalimia. Na ninyi vilevile musalimiane kwa upendo wa kikristo.
Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, aliwapa kitambulisho hiki: “Yule nitakayemubusu ndiye yeye, mumukamate.”
Basi, Esau akakwenda mbio kumupokea Yakobo, akamukumbatia, kumubusu kwenye shingo, na wote wawili wakalia.
Kisha Yakobo akamubusu Rakeli na kulia kwa sauti.
Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.