Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”

Gade chapit la Kopi




Luka 7:39
25 Referans Kwoze  

Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Kwa maana ni ndani ya mutu, ni kusema ndani ya moyo wake, ndimo munamotoka mawazo mabaya yanayoleta: uzinzi, wizi, uuaji,


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Katika kundi lile kulikuwa manunguniko mengi juu yake. Wamoja walisema: “Yeye ni mutu muzuri.” Wengine walisema: “Hapana, si vile, yeye anawadanganya watu.”


Halafu mwanamuke yule akamwambia: “Bwana, ninaona kama wewe ni nabii.


Kwa muda murefu yule mwamuzi alikataa. Lakini kisha akajiuliza mwenyewe: ‘Ijapokuwa mimi simwogopi Mungu wala simujali mutu yeyote,


Yule mulinzi akajiuliza: ‘Sasa nitafanya nini? Bwana wangu ananifukuza kwa kazi. Kulima, mimi siwezi; na kuombaomba, ninasikia haya.


Katika muji ule kulikuwa mwanamuke mumoja aliyejulikana kuwa mwenye mwenendo mubaya. Mwanamuke yule alipopata habari kama Yesu alikuwa akikula ndani ya nyumba ya yule Mufarisayo, akafika akileta chupa la jiwe linalojaa marasi ya bei kali.


Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


maana ndani ya moyo wake anahesabu unachokula. Atakuambia: “Kula, kunywa!” Lakini ndani ya moyo wake hayuko pamoja nawe.


Gehazi, mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu, akasema: “Bwana wangu amemwachilia Namani wa Aramu aende bila kupokea chochote alicholeta. Kama vile Yawe anavyoishi, nitamufuata kusudi nipate kitu kutoka kwake.”


Yeye akawaza na kusema: ‘Nitafanya nini hivi ninakosewa nafasi ya kuwekea mavuno yangu yote?’


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi inavyokuwa vilevile: wanaokuwa wa mwisho watakuwa wa kwanza, nao wanaokuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho.”


Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Akakuja kuinama kwenye miguu ya Yesu, akilia. Machozi yake yakamwangika juu ya miguu ya Yesu, akaipanguza na nywele zake, akaibusu na kuipakaa marasi.


Yesu akamwambia yule Mufarisayo: “Simoni, niko na neno la kukuuliza.” Simoni akajibu: “Mwalimu, sema.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite