Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nanyi munasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki ya walipishaji wa kodi na watenda maovu.’

Gade chapit la Kopi




Luka 7:34
13 Referans Kwoze  

Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Kule wakamutayarishia chakula cha magaribi. Marta aliwashugulikia, na Lazaro alikuwa mumoja wa wale waliokula pamoja na Yesu.


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Siku moja ya Sabato, Yesu aliingia katika nyumba ya mumoja wa wakubwa wa Wafarisayo kwa kula chakula. Mule watu wakabaki wakimuchunguza.


Siku moja Mufarisayo mumoja akamwalika Yesu kwake kuja kula chakula. Basi Yesu akaenda kwenye nyumba ya yule Mufarisayo, na kuikaa kula chakula.


Kisha Lawi akamufanyia Yesu karamu kubwa katika nyumba yake. Walipishaji wengi wa kodi na watu wengine walikuwa wakikula pamoja nao.


Nao Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakawaambia wanafunzi wake: “Kwa sababu gani mwalimu wenu anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Yesu alialikwa vilevile kwenye ndoa ile pamoja na wanafunzi wake.


Yesu alipomaliza kusema, Mufarisayo mumoja akamwalika kwake kuja kula chakula. Yesu akaenda na kuikaa kule.


Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Ni hivi vilevile, Yoane Mubatizaji alikuja, yeye anafunga kula chakula na kunywa divai, nanyi munasema: ‘Yuko na pepo.’


Lakini hekima ya Mungu ilihakikishwa kuwa ya haki na wote wanaoikubali.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite