Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Wale wajumbe wa Yoane walipokwisha kuondoka, Yesu akaanza kuwaambia makundi ya watu habari za Yoane akisema: “Mulienda katika jangwa kuangalia nini? Tete linalotikiswa na upepo? Hapana!

Gade chapit la Kopi




Luka 7:24
14 Referans Kwoze  

Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


nao Anasi na Kayafa walikuwa Makuhani Wakubwa. Halafu Mungu akatoa ujumbe wake kwa Yoane mwana wa Zakaria katika jangwa.


Mutoto yule akakomaa na kuzidi kuwa na nguvu katika roho. Akakaa katika nafasi za jangwa mpaka siku alipojionyesha waziwazi mbele ya Waisraeli.


Basi ninyi wapendwa wangu, mumekwisha kutambua mambo haya. Mujiangalie vizuri kusudi musipotoshwe na makosa ya watu waovu na kukosa kusimama imara.


Wale walimu wa uongo ni kama visima visivyokuwa na maji tena, wao ni kama mawingu yanayopeperushwa na upepo; makao yao yametayarishwa kwenye giza nzito.


Yoane akajibu: “Mimi ni sauti inayotangaza katika jangwa: ‘Munyooshe njia ya Bwana,’ ” sawa vile nabii Isaya alivyosema.


Wewe ni kama maji ya mafuriko. Lakini hautakuwa wa kwanza tena, maana ulipanda juu ya kitanda changu mimi baba yako, wewe ulikichafua; hakika wewe ulipanda juu yake!


Heri mutu yule ambaye sitakuwa kikwazo kwake.”


Basi mulienda kuangalia nini? Mutu aliyevaa nguo nzuri? Hapana! Wale wanaovaa nguo za bei kali na kuishi katika raha wanakaa katika nyumba za kifalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite