Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”

Gade chapit la Kopi




Luka 7:16
31 Referans Kwoze  

Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Watu walipoona jambo hilo wakaogopa na kumusifu Mungu aliyewapa watu mamlaka ya namna ile.


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Wote wakashangaa na kushikwa na woga, wakamutukuza Mungu wakisema: “Leo tumeona mambo ya ajabu.”


Kisha wachungaji wakarudia wakitukuza Mungu na kumusifu kwa ajili ya mambo yote waliyoyasikia na kuyaona, kwa maana yote yalifanyika sawa vile malaika alivyokuwa amewaambia.


Basi watu wote waliokaa karibu naye wakashikwa na woga, na habari ya mambo haya yote ikaenea fasi zote katika inchi ya vilima vya Yudea.


Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli.


Wakaaji wa miisho ya dunia wanashangazwa na vitambulisho vyako. Unasababisha furaha kila pahali, tokea mashariki hata magaribi.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Nao yalimusifu Mungu kwa ajili yangu.


Anania aliposikia maneno hayo, mara moja akaanguka chini na kufa. Na wote waliosikia habari ile wakashikwa sana na woga.


Wafarisayo wakamwuliza tena yule aliyekuwa kipofu: “Na wewe unasema nini juu ya yule aliyekuponyesha macho?” Akajibu: “Yeye ni nabii.”


Watu walipoona kile kitambulisho Yesu alichoonyesha, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye yule nabii aliyepaswa kuja katika dunia!”


Halafu mwanamuke yule akamwambia: “Bwana, ninaona kama wewe ni nabii.


Wakamwuliza Yoane: “Ikiwa wewe si Kristo, wala Elia, wala yule nabii, basi sababu gani unabatiza?”


Halafu wakamwuliza: “Basi wewe ni nani? Wewe ni Elia?” Yoane akajibu: “Mimi si yeye.” Wakamwuliza tena: “Wewe ni yule nabii?” Naye akawajibu: “Hapana.”


Naye akawauliza: “Ni mambo gani?” Nao wakamujibu: “Haujui mambo yaliyomupata Yesu wa Nazareti? Yeye alishuhudiwa na Mungu na watu wote kwamba alikuwa nabii mwenye uwezo katika mambo aliyofanya na kusema.


Nao wakajibu: “Wamoja wanasema kwamba wewe ni Yoane Mubatizaji, wengine wanasema kwamba wewe ni Elia, na wengine wanasema kwamba wewe ni mumoja wa manabii wa zamani aliyefufuka.”


Halafu watu wote wa inchi ya Wagerasi wakashikwa na woga mukubwa, kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke kwao. Basi Yesu akaingia ndani ya chombo, kusudi apate kuondoka kule.


Simoni Petro alipoona mambo hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu na kusema: “Bwana, utoke karibu nami, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi!”


Basi wale wanawake wakaondoka upesi kutoka kwenye kaburi, wakijazwa na woga na furaha kubwa vilevile. Wakakimbia kwenda kuwapasha wanafunzi wake habari ile.


Ni yule yule Musa ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: ‘Mungu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu.’


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Halafu yule aliyekuwa maiti akaamuka, akaikaa na kuanza kusema. Na Yesu akamurudisha kwa mama yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite