Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha akajongea, akagusa sanduku, nao watu waliokuwa wakilibeba wakasimama. Akasema: “Kijana, ninakuamuru, amuka!”

Gade chapit la Kopi




Luka 7:14
20 Referans Kwoze  

Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Yesu akamwambia: “Mimi ni ufufuko na uzima, kwa maana anayeniamini, ataishi tena hata ikiwa amekufa.


Kisha Elia akajinyoosha juu ya mutoto yule mara tatu na kumwomba Yawe: “Ee Yawe, Mungu wangu, umurudishie mutoto huyu roho yake!”


Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Nimekuweka kuwa babu wa mataifa mengi.” Abrahamu alimwamini Mungu, kwa hiyo yeye ni baba yetu mbele yake. Ni yeye Mungu anayewafufua wafu na kuamuru vitu visivyokuwa vipate kuwa.


Kwa maana kama vile Baba anavyofufua wafu na kuwarudishia uzima, vile vile Mwana anawapa uzima wale anaowataka.


Wafu wako wataishi tena, miili yao itafufuka. Wanaolala katika mavumbi wataamuka na kuimba kwa furaha! Mungu atapeleka umande wake wa uzima, nao wanaokuwa kwa wafu watatoka wazima.


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.


ndivyo mutu anavyokufa, wala haamuki tena. Hataamuka tena wala kusisimuka, hata pale mbingu zitakapotoweka.


(Kwa maana ni haya kusema juu ya mambo watu hao wanayofanya kwa siri.)


Yawe akasikiliza ombi la Elia. Mutoto akaanza kupumua tena.


Akashika mukono wa mutoto, akamwambia: “Talita kumu,” maana yake: “Kijana binti, ninakuambia, amuka!”


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


Halafu yule aliyekuwa maiti akaamuka, akaikaa na kuanza kusema. Na Yesu akamurudisha kwa mama yake.


Na jambo hili Yesu alilolifanya likaenea katika Yudea yote na katika inchi zote zinazokuwa pembeni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite