Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 6:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Kama mutu akikupiga kofi kwa shavu moja, umugeuzie lingine vilevile. Kama mutu akikunyanganya koti yako, umwachie shemizi yako vilevile.

Gade chapit la Kopi




Luka 6:29
15 Referans Kwoze  

Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Munavumilia hata mutu anayewatia katika utumwa, anayeiba mali zenu, anayewagandamiza, anayewazarau na anayewapiga kofi kwenye uso.


Kweli mambo haya ya kuwa na mashitaki kati yenu yanahakikisha kwamba mumeshindwa kabisa. Si ingekuwa vizuri zaidi kwenu kuvumilia ubaya? Si ingekuwa vizuri zaidi kunyanganywa mali zenu?


Yesu aliposema maneno haya, mumoja wa walinzi waliokuwa karibu naye, akamupiga kofi, akisema: “Ni hivi unavyopaswa kumujibu Kuhani Mukubwa?”


Halafu wamoja wakamutemea mate juu ya uso, na kumupiga ngumi. Na wengine wakamupiga makofi,


Inamupasa kumugeuzia shavu mwenye kumupiga, na kuwa tayari kupokea matusi yake.


Wale walionipiga, niliwaelekezea mugongo wangu, wale walioziongoa ndevu zangu, mashavu yangu. Sikuficha uso wangu wakati watu waliponitukana na kunitemea mate.


Hata sasa, tunateswa na njaa na kiu, tunakosa nguo, tunapigwa, tunatangatanga bila makao.


Walimufunika uso kwa kitambaa na kumwuliza: “Tambua sasa, ni nani aliyekupiga?”


Paulo aliposema maneno hayo, Kuhani Mukubwa Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wamupige kofi kwenye kinywa.


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Kisha nabii Zedekia mwana wa Kenana akamukaribia Mikaya, akamupiga kofi kwenye shavu na kumwuliza: “Kwa njia gani Roho wa Yawe ameniacha na akakuja kusema nawe?”


Mufalme akamwambia: “Usiniambie zaidi juu ya mambo yako pekee. Mimi nimekwisha amua kuwa wewe pamoja na Siba mutagawanyana inchi ya Saulo.”


Mutu akikuomba kitu umupe nacho, na anayekunyanganya vitu vyako, usiombe akurudishie.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite