Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 6:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Watu wote walitaka kumugusa, kwa sababu uwezo ulikuwa ukitoka ndani yake na kuwaponyesha wote.

Gade chapit la Kopi




Luka 6:19
15 Referans Kwoze  

na kumusihi awaruhusu waguse hata upindo wa nguo yake tu. Nao wote waliougusa walipona.


Watu waliokuwa na magonjwa walikuwa wakisukumana kusudi wamufikie na kumugusa kwa maana aliwaponyesha watu wengi.


Na kila pahali Yesu alipokwenda, katika vijiji, miji, au kwenye mbuga, watu waliweka wagonjwa katika viwanja vya makutano na kumusihi awaache wagonjwa waguse hata upindo wa kanzu yake tu. Nao wote waliougusa, walipona.


Na mara moja Yesu akatambua kama nguvu zilitoka ndani yake. Basi akageuka kati ya kundi na kuuliza: “Ni nani aliyegusa nguo yangu?”


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Yesu na wanafunzi wake wakafika Betesaida. Kule wakamuletea Yesu mutu mumoja kipofu na kumwomba amuguse kusudi apate kupona.


Na hata watu walitwaa vitambaa na nguo zilizogusa mwili wa Paulo, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakapona na pepo wakatoka ndani yao.


Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria waliotoka katika kila kijiji cha jimbo la Galilaya na la Yudea na toka Yerusalema, walikuwa wakiikaa pale. Naye alikuwa akiponyesha wagonjwa kwa uwezo wa Bwana.


Siku moja, wakati wa mazishi, watu waliona moja kati ya makundi yale. Wakatupa maiti katika kaburi la Elisha na kukimbia. Mara tu maiti hiyo ilipogusa mifupa ya Elisha, ilifufuka na kusimama wima.


Watu hao walikuja kumusikiliza na kuponyeshwa magonjwa yao. Na wale walioteswa na pepo waliponyeshwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite