Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 6:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kulipokucha, akawaita wanafunzi wake, na kuchagua hawa kumi na wawili katikati yao, akawapanga jina la mitume:

Gade chapit la Kopi




Luka 6:13
20 Referans Kwoze  

Na ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa umejengwa juu ya mawe ya musingi kumi na mawili na juu ya kila jiwe kulikuwa kumeandikwa jina la kila mumoja wa mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.


Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.


Mitume wakarudi kwa Yesu, na kumwelezea mambo yote waliyofanya na yote waliyofundisha.


Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Kisha kukaonekana kitambulisho kikubwa mbinguni. Kulikuwa mwanamuke aliyekuwa amefunikwa na jua, na mwezi chini kwenye miguu yake. Na juu ya kichwa kulikuwa taji lenye nyota kumi na mbili.


Ninataka mukumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi muliyotolewa na mitume wenu.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Kwa sababu hii, Mungu anasema katika hekima yake: ‘Nitawatumia manabii na mitume; watawaua wamoja kati yao na kuwatesa wengine wao.’


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.


Na haya ndiyo majina ya hao mitume wake kumi na wawili: kwanza Simoni (anayeitwa vilevile Petro) na ndugu yake Andrea; Yakobo na ndugu yake Yoane, ambao ni wana wa Zebedayo;


Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,


Basi wanafunzi wakaanza kuulizana: “Kuna mutu aliyemuletea chakula?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite