Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 5:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Halafu Yesu akitambua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munajiuliza mambo hayo yote?

Gade chapit la Kopi




Luka 5:22
15 Referans Kwoze  

Lakini Yesu akawaambia: “Kwa sababu gani munafazaika na kuwa na mashaka?


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Yesu akatambua maneno waliyosema, basi akawauliza: “Sababu gani munasemezana juu ya kukosa mikate? Hamujafahamu wala kuelewa? Mioyo yenu ingali migumu?


Yesu akitambua mafikiri yao, akawaambia: “Watu wa ufalme wowote wakigombana wao kwa wao, ufalme ule utaanguka. Nao wakaaji wa muji wowote au watu wa jamaa yoyote wakigombana wao kwa wao, muji ule au jamaa ile haitadumu.


Naye Yesu akijua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munawaza maneno hayo mabaya?


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Nikiikaa au nikisimama, wewe unajua; wewe unajua kila kitu ninachofikiri juu yake.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile, utaanza kuwaza ndani ya moyo wako na kupanga mipango miovu na kusema:


Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maneno mema yanamufurahisha.


Yesu alipojua habari ile, akaondoka kule. Watu wengi wakamufuata, naye akawaponyesha wagonjwa wote.


Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”


Kitu gani kinachokuwa chepesi, kusema: ‘Zambi zako zimesamehewa,’ au kusema: ‘Simama, utembee?’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite