Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 5:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”

Gade chapit la Kopi




Luka 5:21
23 Referans Kwoze  

Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Wayuda wakamujibu: “Hatutaki kukutupia mawe kwa ajili ya tendo zuri, lakini kwa sababu unamutukana Mungu. Wewe ni mutu tu, lakini unajifanya kuwa Mungu!”


Na waalikwa wengine waliokuwa wakikula pamoja na Yesu, wakaanza kujisemesha: “Ni mutu gani huyu anayesamehe zambi?”


Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.


Kisha niliitikia makosa yangu mbele yako, wala sikuficha uovu wangu. Nilisema kwamba nitaungama makosa yangu mbele ya Yawe. Nawe ukanisamehe zambi yangu.


Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.


Ni nani anayeweza kuwashitaki watu ambao Mungu alijichagulia? Hakuna hata mumoja! Mungu peke yake amewahesabia haki mbele yake.


Ee Yawe, utusikie; utusamehe ee Yawe. Ee Yawe, kwa ajili ya heshima yako utusikie na utende, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya muji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Lakini kwako tunapata usamehe, kusudi sisi tukuheshimu.


Ananisamehe uovu wangu wote, na kuniponyesha magonjwa yote.


Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria waliotoka katika kila kijiji cha jimbo la Galilaya na la Yudea na toka Yerusalema, walikuwa wakiikaa pale. Naye alikuwa akiponyesha wagonjwa kwa uwezo wa Bwana.


Halafu walimu wamoja wa Sheria waliokuwa pale wakajisemesha: “Mutu huyu anamutukana Mungu!”


Utatuhurumia tena; utatupilia mbali zambi zetu, utazitupa zote katika vilindi vya bahari.


Wakuwe kama maganda yanayopeperushwa na upepo, wakikimbizwa na malaika wa Yawe!


Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Musianze tu kujisemesha kwamba Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


Halafu Yesu akitambua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munajiuliza mambo hayo yote?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite