Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 5:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria waliotoka katika kila kijiji cha jimbo la Galilaya na la Yudea na toka Yerusalema, walikuwa wakiikaa pale. Naye alikuwa akiponyesha wagonjwa kwa uwezo wa Bwana.

Gade chapit la Kopi




Luka 5:17
20 Referans Kwoze  

Watu wote walitaka kumugusa, kwa sababu uwezo ulikuwa ukitoka ndani yake na kuwaponyesha wote.


Lakini Yesu akasema: “Kuna mutu aliyenigusa kwa maana nimejisikia kwamba nguvu zimenitoka.”


Mungu akaendelea kufanya miujiza ya ajabu kwa njia ya Paulo.


vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Utumie nguvu zako kwa kuponyesha watu, kwa kufanya maajabu na vitambulisho kwa uwezo wa jina la mutumishi wako mutakatifu Yesu.”


Wafarisayo na walimu wamoja wa Sheria waliotoka Yerusalema wakakusanyika mbele ya Yesu.


Na mara moja Yesu akatambua kama nguvu zilitoka ndani yake. Basi akageuka kati ya kundi na kuuliza: “Ni nani aliyegusa nguo yangu?”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakamufikia Yesu kutoka Yerusalema. Basi wakamwuliza:


Lakini anayeshika ukweli, anakuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yaonekane wazi kwamba yanatendeka sawa Mungu anavyoamuru.”


Nyuma ya siku tatu, wakamukuta ndani ya hekalu, akiikaa katikati ya walimu wakubwa wa Sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maulizo.


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Lakini Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria walikataa mupango wa Mungu juu yao, na kukataa kubatizwa na Yoane.)


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”


wakishika nyoka au kunywa sumu yoyote, hawatakufa. Wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”


Walimu wa Sheria waliotoka Yerusalema, wakasema hivi juu ya Yesu: “Amepatwa na Belzebuli.” Na wengine wao wakasema: “Ni huyo mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”


Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.


Yesu akamujibu: “Wewe unayekuwa mwalimu mukubwa katika inchi ya Israeli, haujui maneno haya?


Lakini Mufarisayo mumoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimiwa sana na watu wote, akasimama katika baraza na kuamuru mitume wapelekwe inje kwa muda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite