Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akapona ukoma.

Gade chapit la Kopi




Luka 5:13
15 Referans Kwoze  

Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.


Basi, Namani akateremuka kwenye muto Yordani akajitumbukiza mule mara saba, kama alivyoagizwa na Elisha mutu wa Mungu, naye akapona kabisa. Ngozi yake ikakuwa laini na yenye afya kama ya mutoto mudogo.


Basi akainama kunapokuwa yule mama, akaamuru ile homa itoke ndani yake, naye akapona. Na mara moja akasimama na kuanza kuwashugulikia.


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Elisha akamutuma mutumishi wake amwambie: “Kwenda uoge mara saba katika muto Yordani, nawe utapona kabisa.”


Mungu akasema: “Maji yanayokuwa chini ya mbingu yakusanyike pahali pamoja, inchi kavu itokee.” Ikakuwa hivyo.


Mungu akasema: “Mwangaza ukuwe.” Mwangaza ukakuwa.


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.


Yesu alipokuwa katika muji mumoja kati ya miji ile, kukatokea mutu aliyejaa na ukoma mwili wote. Naye alipomwona Yesu, akainama uso mpaka chini, akamusihi akisema: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”


Yesu akamwamuru hivi: “Usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite