Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 na kumwambia: “Nitakupa falme hizo zote zenye uwezo na utukufu, kwa maana mimi nimezipewa zote, nami ninaweza kuzitoa kwa mutu yeyote ninayetaka.

Gade chapit la Kopi




Luka 4:6
15 Referans Kwoze  

Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Sitasema nanyi maneno mengi tena, kwa sababu mutawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu,


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watu wa Mungu na kuwashinda. Akapewa hata mamlaka ya kutawala watu wote, wa kila kabila, kila jamaa, kila luga na kila taifa.


Yule nyama niliyemwona alifanana na chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Yule nyoka mukubwa akamupa uwezo wake pamoja na kiti chake cha kifalme na mamlaka makubwa.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Wanadamu wote ni kama majani. Na utukufu wao wote unatoweka kama maua. Majani yanakauka na maua yanaanguka.


Na jambo hilo si la kushangaza kwa maana Shetani mwenyewe anajisingizia kuwa malaika wa mwangaza.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa, imepanua kinywa chake mpaka mwisho. Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema wanaingia humo makundi kwa makundi, vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.


Halafu akaanza kueleza juu ya utajiri anaokuwa nao, wana anaokuwa nao, jinsi mufalme alivyomupandisha cheo, na jinsi alivyopewa madaraka zaidi kuliko wakubwa wengine wote wa mufalme.


Basi ukiinama mbele yangu kwa kuniabudu, zote zitakuwa zako.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite