Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Yesu akafika Nazareti, nafasi alipokomalia. Siku ya Sabato ilipotimia akaingia katika nyumba ya kuabudia kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama kwa kusoma Maandiko Matakatifu;

Gade chapit la Kopi




Luka 4:16
14 Referans Kwoze  

Na sawa ilivyokuwa desturi, Paulo akaingia katika nyumba ile. Kwa muda wa siku tatu za Sabato zilizofuatana juma kwa juma, akabishana na watu waliokuwa mule, akitumia Maandiko Matakatifu.


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Basi Yesu akarudia Nazareti pamoja nao, akaendelea kuwatii. Na mama yake alichunga maneno haya yote katika moyo wake.


Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, akaenda pamoja nao kule kwa sikukuu ile kama ilivyokuwa desturi.


Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.


Halafu akaanza kuwaambia: “Maandiko haya yametimia leo.”


Wakati wazazi wa Yesu walipokwisha kutimiza kanuni zote zilizoagizwa na Sheria ya Bwana, wakarudia pamoja naye Galilaya, katika muji wao wa Nazareti.


Alifundisha katika nyumba zao za kuabudia, na kusifiwa na watu wote.


wakamupa kitabu cha nabii Isaya. Halafu akakifungua na kupata nafasi inayoandikwa:


Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite