Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Halafu watu wengi walimufikia Yoane kusudi awabatize. Naye aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliwaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?

Gade chapit la Kopi




Luka 3:7
12 Referans Kwoze  

Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.


Munatoa mayai ya nyoka yenye sumu, munafuma wavu wa buibui. Anayekula mayai yenu anakufa, na yakipasuliwa, nyoka anatokea ndani yake.


Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


na kusema: “Wewe mutoto wa Shetani unayejaa udanganyifu na ukorofi wa kila namna! Wewe usiyependa kuona jambo la haki! Wewe hauchoki na kugeuza maneno ya ukweli ya Bwana!


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Waliungama zambi zao, naye Yoane aliwabatiza katika muto Yordani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite