Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi Yoane akapita katika inchi zote zinazokuwa pembeni ya muto Yordani, akihubiri. Akawaambia watu wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawaondolea zambi.

Gade chapit la Kopi




Luka 3:3
12 Referans Kwoze  

Upate kuwajulisha watu wake kwamba atawaokoa akisamehe zambi zao.


Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”


Paulo akawaambia: “Yoane aliwabatiza wale waliogeuka toka zambi zao na kuwaambia Waisraeli kwamba wamwamini yule atakayekuja nyuma yake, naye ndiye Yesu.”


Mbele Yesu hajajionyesha, Yoane alihubiri kwa Waisraeli wote kwamba wageuke toka zambi zao na kubatizwa.


Basi wakamwendea Yoane na kumwambia: “Mwalimu, unakumbuka yule mutu aliyekuwa pamoja nawe ngambo ya Yordani, yule uliyemushuhudia? Angalia sasa, yeye anabatiza, na watu wote wanamufikia!”


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Mambo hayo yalifanyika Betania, ngambo ya muto Yordani, pahali Yoane alipokuwa akibatiza.


Atawageuza Waisraeli wengi kwa kumurudilia Bwana Mungu wao.


Yesu, akarudia toka kwenye muto Yordani, akijazwa na Roho, na Roho huyo akamwongoza kwenda katika jangwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite