Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 24:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Lakini wakamusihi sana abakie pamoja nao, kwa maana ilikuwa magaribi na giza lilitaka kuingia. Basi akaingia ndani ya nyumba kubakia pamoja nao.

Gade chapit la Kopi




Luka 24:29
6 Referans Kwoze  

Siku moja Elisha alikwenda Sunemu, ambako kulikuwa mama mumoja tajiri. Mama yule akamwalika Elisha kwa chakula, na toka siku hiyo ikakuwa kawaida Elisha kula chakula kwake kila mara alipopitia kule.


Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.


Halafu bwana wake akamwambia: ‘Kwenda katika njia kwenye vijiji na pembeni ya mashamba, uwalazimishe watu wafike kuingia, kusudi nyumba yangu ipate kujaa.


Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.


Nao walipofika karibu na kile kijiji ambamo walikuwa wakienda, Yesu akaendelea mbele, akiwa sawa mwenye kuwaacha.


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite