47 Mukubwa wa waaskari alipoona mambo yale yaliyotokea, akamusifu Mungu, akisema: “Hakika mutu huyu alikuwa mwenye haki!”
Mukubwa wa waaskari aliyekuwa akisimama mbele ya Yesu, alipoona namna alivyokata roho, akasema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Sisi tunahukumiwa kwa haki, kwa maana tunaazibiwa kufuatana na matendo yetu mabaya. Lakini mutu huyu hakufanya ubaya wowote.”
Watu walipoona jambo hilo wakaogopa na kumusifu Mungu aliyewapa watu mamlaka ya namna ile.
Wayuda wakamujibu: “Kufuatana na moja ya sheria zetu, mutu huyu anapaswa kuuawa, kwa sababu alijiita Mwana wa Mungu.”
Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,