Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 23:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Walipowafikisha kwenye pahali palipoitwa “Kilima cha Mufupa wa Kichwa,” wakamutundika Yesu juu ya musalaba. Vilevile walitundika wale watenda maovu, mumoja kwa upande wa kuume wa Yesu na mwingine kwa upande wa kushoto.

Gade chapit la Kopi




Luka 23:33
19 Referans Kwoze  

Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


(Ilifanyika hivi kusudi litimie lile neno Yesu alilosema kwa kuonyesha kifo gani atakachokufa.)


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Na wakati walipokwisha kutimiza yote yaliyoandikwa juu yake, wakamushusha toka juu ya musalaba na kumuzika.


Mungu wa babu zetu alimufufua Yesu, yule ninyi muliyemwua kwa kumutundika juu ya musalaba.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Sawa Musa alivyonyanyua nyoka ya shaba juu ya muti katika jangwa, ni hivi vilevile, sherti Mwana wa Mutu anyanyuliwe,


Aliwaambia kwamba Mwana wa Mutu anapaswa kutolewa katika mikono ya wenye zambi, na kutundikwa juu ya musalaba, lakini kwa siku ya tatu kisha kufa, atafufuka.”


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Nao watamuchekelea, watamupiga fimbo na kumutundika juu ya musalaba. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Koo langu limekauka kama kigae; ulimi wangu unanata ndani ya kinywa changu. Wewe umenilaza pembeni ya kaburi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite