3 Basi Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ndiwe mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Ni wewe ndiwe umesema.”
Mbele ya Mungu anayevipatia vitu vyote uzima, na mbele ya Kristo Yesu aliyetoa ushuhuda wa kweli mbele ya Pontio Pilato, ninakuagiza maneno haya:
Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”
Wote wakamwuliza: “Basi, wewe ni Mwana wa Mungu?” Yesu akawajibu: “Ninyi munasema kwamba mimi ndiye.”
Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ni Mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Umesema.”
Wakafika kila wakati mbele yake na kusema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda.” Nao wakamupiga makofi.
Na mashitaki haya yalikuwa yameandikwa juu ya musalaba wake: “Huyu ndiye Mufalme wa Wayuda.”
Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.
Kisha wakaanza kumusalimia, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”
Yesu alipopelekwa mbele ya liwali, yeye akamwuliza: “Wewe ndiwe Mufalme wa Wayuda?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema.”
Kwa hiyo Pilato akawakuta inje, na kuwauliza: “Munamushitaki mutu huyu juu ya nini?”