24 Halafu akakata shauri la kuwatendea sawa walivyotaka.
Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.
Basi Pilato akawafungulia Baraba, lakini akaamuru wamupige Yesu fimbo na kumutoa kusudi atundikwe juu ya musalaba.
Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.
Kwa kuwa Pilato alitaka kuwapendeza watu, basi akawafungulia Baraba. Na kisha kuamuru wamupige Yesu fimbo, akamutoa kusudi atundikwe juu ya musalaba.
Halafu Pilato akaamuru wamukamate Yesu na kumupiga fimbo.
Lakini wakaendelea kupiga kelele kubwa wakiomba Yesu atundikwe juu ya musalaba. Na kwa mwisho akashindwa kwa sababu ya makelele yao.
Akamufungua yule mutu waliyetaka, aliyefungwa kwa ajili ya kuleta fujo na kuua watu, na kumutoa Yesu kwao kusudi wamutendee vile walivyotaka.