18 Lakini wote pamoja wakapiga kelele wakisema: “Umwue mutu huyu na utufungulie Baraba!”
Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”
Maana wote walimufuata nyuma wakilalamika: “Auawe!”
Yeye alikuwa Mutakatifu na Mwenye Haki, lakini mukamukana, mukataka Pilato awafungulie mwuaji.
Kila sikukuu ya Pasaka, Pilato alipaswa kuwafungulia watu mufungwa mumoja.]
(Baraba alikuwa amefungwa kwa ajili ya fujo iliyofanyika katika muji na kwa ajili ya kuua watu.)
Lakini Petro alisimama inje karibu na mulango. Yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na Kuhani Mukubwa, akatoka inje, akasema na mwanamuke aliyelinda mulango, naye akamwachilia Petro kuingia ndani.