Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 22:61 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

61 Bwana akageuka na kumwangalia Petro. Petro akakumbuka maneno yale Bwana aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika atakuwa amemukana mara tatu.

Gade chapit la Kopi




Luka 22:61
19 Referans Kwoze  

Yesu akamujibu: “Ninakuambia wewe Petro kwamba leo, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu kuwa haunijui.”


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Atashangilia mbele ya watu na kusema: “Nilitenda zambi na kupotosha usawa, nami sikuazibiwa kutokana na hayo.


Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.


Basi mukumbuke namna mulivyokuwa zamani ninyi munaokuwa kwa kizalikio watu wa mataifa mengine. Wayuda wanawaita ninyi watu wasiotahiriwa, lakini wao wanajiita wenye kutahiriwa kwa sababu ya kitambulisho cha kutahiriwa na watu katika miili yao.


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Yesu akamujibu: “Hakika wewe ni tayari kutoa maisha yako kwa ajili yangu? Kweli, kweli ninakuambia: mbele jogoo hajawika, utakuwa umekwisha kunikana mara tatu.”


Bwana akamujibu: “Marta! Marta! Kwa nini unahangaika na kusumbuka kwa ajili ya vitu vingi?


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


Na mara moja Yesu akatambua kama nguvu zilitoka ndani yake. Basi akageuka kati ya kundi na kuuliza: “Ni nani aliyegusa nguo yangu?”


naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia kwamba katika usiku huu, mbele jogoo hajawika utakuwa umenikana mara tatu.”


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


na kuwatuma kwa Bwana kumwuliza: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”


Lakini Petro akasema: “Sijui mambo unayoyasema.” Wakati ule alipokuwa angali akisema, jogoo akawika.


Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite