45 Kisha kuomba, alirudia pahali alipoacha wanafunzi wake, akawakuta wamelala kwa sababu walikuwa na huzuni.
Aliporudi tena, akawakuta wanafunzi wale wamelala usingizi, kwa maana macho yao yalikuwa yamewezwa sana na usingizi.
Kisha akarudi pahali pale alipowaacha wale wanafunzi, akawakuta wamelala usingizi. Akamwambia Petro: “Hamukuweza kukesha pamoja nami hata kwa saa moja tu?
Aliporudi akawakuta wamelala usingizi. Akamwambia Petro: “Simoni, umelala? Haukuweza kukesha hata kwa saa moja tu?
Yesu alikuwa katika uchungu mukubwa, akazidi kuomba kwa bidii. Jasho iliyomutoka ikakuwa kama matone ya damu yaliyokuwa yakitiririka mpaka chini.]
Akawaambia: “Sasa, ninyi munalala? Muamuke na muombe, kusudi musianguke katika majaribu.”