Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 22:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Alipofika kwenye nafasi ile, akawaambia: “Muombe kusudi musianguke katika majaribu.”

Gade chapit la Kopi




Luka 22:40
16 Referans Kwoze  

Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Akawaambia: “Sasa, ninyi munalala? Muamuke na muombe, kusudi musianguke katika majaribu.”


Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake.


Utusamehe zambi zetu, maana sisi vilevile tunawasamehe wote wanaotukosea, usituache kuingia katika majaribu.’ ”


Uniimarishie hatua zangu kama ulivyoahidi; usikubali mimi nitawaliwe na uovu.


Nimefuata siku zote njia yako; wala sijatereza hata kidogo.


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Lakini nani anayeona makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, unisamehe makosa nisiyoyajua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite