Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 22:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yesu akatoka na kwenda kwa mulima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake. Na wanafunzi wake wakamufuata.

Gade chapit la Kopi




Luka 22:39
10 Referans Kwoze  

Yesu alikuwa akipitisha muchana katika hekalu akihubiri, na usiku alikuwa akienda kulala kwenye mulima wa Mizeituni.


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema upande wa kijiji cha Betefage, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,


Na walipokwisha kuimba wimbo, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


Yesu alipokuwa akiikaa kwa mulima wa Mizeituni kuelekea upande wa hekalu, Petro, Yakobo, Yoane na Andrea walipokuwa peke yao pamoja naye, wakamwuliza:


Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.


Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.


Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite