15 Akawaambia: “Nimetamani sana kula karamu hii ya Pasaka pamoja nanyi mbele ya kuteswa kwangu!
Niko na muzigo wa mateso ninaopaswa kubeba, nami ninasongwa sana mpaka mapaswa hayo yatakapotimizwa!
Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.
Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.
Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.
Saa ilipotimia, Yesu akaikaa kula chakula pamoja na wanafunzi wake.
Kwa maana ninawaambia, sitakula tena karamu hii ya Pasaka mpaka siku ile nitakapokula ile yenye kukamilika katika Ufalme wa Mungu.”