Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 21:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 “Kutakuwa siku vitu hivi munavyoona vitabomolewa, wala hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine.”

Gade chapit la Kopi




Luka 21:6
20 Referans Kwoze  

Yesu akamujibu: “Unaona majengo haya makubwa? Hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


Lakini Yesu akawaambia: “Munaona haya yote? Kweli ninawaambia: hapa hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


Maana mulima Sayuni umeachwa utupu, mbweha wanazungukazunguka humo.


Yawe atayakusanya mataifa yote kwa kuushambulia Yerusalema. Muji utakamatwa, nyumba zenu zitatekwa, na wanawake wenu watakamatwa kwa kinguvu. Nusu ya wakaaji wa muji watapelekwa katika uhamisho, lakini nusu itakayobaki haitaondoshwa inje ya muji.


Fungua milango yako, ewe Lebanoni kusudi moto uiteketeze mierezi yako!


Namna gani zahabu yetu ilivyochakaa, zahabu safi kabisa ilivyobadilika! Mawe ya bei kali yamesambazwa kwa barabara zote.


Katika siku Hezekia alipokuwa mufalme wa Yuda, Mika wa Moreseti aliwatangazia watu wote kwamba Yawe wa majeshi alisema hivi: Sayuni utalimiwa kama shamba, Yerusalema utabaki mabomoko, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Kwa nini umetabiri kwa jina la Yawe, ukisema kwamba nyumba hii itaharibiwa kama ile ya Shilo na muji huu utakuwa ukiwa, bila wakaaji? Na watu wote wakamuzunguka Yeremia katika nyumba ya Yawe.


basi, nitaiharibu nyumba hii kama nilivyoharibu ile ya Shilo, na nitaufanya muji huu kuwa mufano kwa mataifa yote ya dunia yatakaoutumia kwa kutoa laana.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Halafu wakamwuliza: “Mwalimu, mambo hayo unayotoka kusema yatakuwa wakati gani? Na ni kitambulisho gani kitakachoonyesha kwamba yanataka kutimia?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite