Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 21:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Yesu alikuwa akipitisha muchana katika hekalu akihubiri, na usiku alikuwa akienda kulala kwenye mulima wa Mizeituni.

Gade chapit la Kopi




Luka 21:37
15 Referans Kwoze  

Yesu akatoka na kwenda kwa mulima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake. Na wanafunzi wake wakamufuata.


Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.


Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.


Kisha akawaacha, akatoka inje ya muji wa Yerusalema, naye akaenda Betania na kulala kule.


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema upande wa kijiji cha Betefage, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,


Kisha mitume wakarudi Yerusalema tokea kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa karibu na muji huo kwenye umbali wa yapata kilometre moja.


Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.


Alipokaribia Yerusalema kwenye mutelemuko wa mulima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wakafurahi na kuanza kumusifu Mungu kwa sauti kubwa kwa ajili ya miujiza yote waliyoiona.


Kesho yake, walipotoka Betania, Yesu akasikia njaa.


Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.


Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”


Alipokaribia kufika katika kijiji cha Betefage na cha Betania upande wa mulima wa Mizeituni, Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake, akiwaambia:


Yesu alikuwa akifundisha kila siku ndani ya hekalu. Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wakubwa wa watu wakatafuta kumwua.


Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alijua pahali pale, kwa sababu Yesu alikuwa akikutana kule mara nyingi pamoja na wanafunzi wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite