Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 21:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kwa maana siku zile zitakuwa siku za azabu ya Mungu, kusudi mambo yote yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yatimie.

Gade chapit la Kopi




Luka 21:22
22 Referans Kwoze  

Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.


Lakini kwa nguvu ya neno lile lile, mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa kuteketezwa kwa moto. Zinalindwa kwa ajili ya Siku ile ambayo watu wabaya watahukumiwa na kuangamizwa.


Niliamua kwamba siku ya kulipiza kisasi imefika; wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.


Maana Yawe yuko na siku ya kulipiza kisasi; mwaka wa kulipiza waadui za Sayuni.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Mambo hayo yote yalitukia kusudi yatimie maneno Bwana aliyosema kwa njia ya nabii:


Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Enyi mataifa, mushangilie watu wake, maana yeye analipiza kisasi damu ya watumishi wake, anawalipiza kisasi wapinzani wake, na kuitakasa inchi ya watu wake.


Sina njia ya kuwaazibu? Silaha zangu ziko katika mukono wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite