Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 21:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 “Wakati mutakapoona muji wa Yerusalema umezungukwa na waaskari, mujue kwamba uharibifu wake unakaribia.

Gade chapit la Kopi




Luka 21:20
7 Referans Kwoze  

Kwa maana siku zitakufikia wakati waadui zako watakapokuzunguka kwa vita, watakapojenga ukuta wa kujikingia pembeni yako, na kukusonga pande zote.


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


Mutawala huyo atafanya mapatano imara na watu wengi kwa muda wa miaka saba. Kisha nusu ya muda huo atakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Pahali pa juu katika hekalu patasimamishwa chukizo linaloleta uharibifu, nalo litabaki pale mpaka yule aliyemusimamisha atakapoangamizwa kama ilivyopangwa na Mungu.


Halafu wakamwuliza: “Mwalimu, mambo hayo unayotoka kusema yatakuwa wakati gani? Na ni kitambulisho gani kitakachoonyesha kwamba yanataka kutimia?”


“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)


Kwa njia ya imani, ukuta uliozunguka muji Yeriko ulianguka wakati Waisraeli walipokwisha kuuzunguka kwa muda wa siku saba.


Nasi vilevile tunazungukwa na kundi kubwa kama lile la wale walioshuhudia imani yao. Basi tutupilie mbali vitu vyote vinavyotusonga, nazo zambi zinazotufunga upesi na tukimbie kwa juhudi sana katika mashindano tunayowekewa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite